25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Mazungumzo ya mwisho Sudan leo

KHARTOUM,SUDAN

MAZUNGUMZO ya kutatua masuala yaliyobaki kati ya waandamanaji wa Sudan na watawala wa kijeshi yanatarajiwa kuanza leo.

Hayo yanajiri wakati waandamanaji kadhaa wakimiminika mitaani mjini Khartoum kuitisha uchugunzi huru kuhusiana na ukandamizaji mkubwa uliofanywa dhidi ya kambi ya maandamano mwezi Juni. 

Pande hizo mbili tayari zimesaini makubaliano ya kugawana madaraka ambayo yanalenga kuunda baraza tawala la pamoja la kijeshi na kiraia ambalo litapisha utawala wa kiraia. 

Mpatanishi wa Umoja wa Afrika, Mohamed El Hacen Lebatt, amesema katika taarifa kuwa pande zote mbili zimealikwa kushiriki mazungumzo ya mwisho kuhusu tamko la kikatiba. 

Mazungumzo hayo yatahusu masuala kama vile mamlaka ya baraza tawala litakaloundwa, kutumika kwa vikosi vya usalama na kinga ya majenerali kutokana na machafuko yanayohusiana na maandamano.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles