27.6 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Mashabiki wa ndondi Kigogo waahidi kutembea kwa miguu hadi Morogoro

Na Winfrida Mtoi, Mtanzania Digital

Mashabiki wa bondia Lutengano John kutoka Kigogo mwisho na Mburahati, wameahidi kutembea kwa miguu kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro kuhakikisha mpinzani wao Ally Mazome anapigika mapema katika pambano lililopewa jina la Hatukimbii Hatuogopi litakalofanyika siku ya Eid Pili mkoani humo.

Wakizungumzia safari hiyo, wamesema lengo la kufanya hivyo ni kwenda kumsapoti na kumhamasisha bondia wao Lutengano ili aweze kupata ushindi wa mapema dhidi ya mpinzani katika raundi ya tatu ya pambano.

“Lutengano ni bondia anaiwakilisha Kigogo na Dar es Salaam kwa ujumla. Tumuambie Ally Mazome afanye mazoezi kama anabeba viroba awe analima magimbi, mihogo, sisi tunaamini Mburahati haijawahi kutuzingua.

“Sisi hapa kwa ajili ya kumfuata Mazome, hatupandi gari, tunatembea kwa mguu,” wametamba mashabiki ambao ni Singa One na Ibada Jafar.

Kwa upande wake Lutengano amesema anajiandaa vizuri kuhakikisha snamaliza pambano hilo mapema katika raundi ya tatu ya mchezo kwa kuwapa burudani ya masumbwi mashabiki zake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles