23.6 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Marekani, China zatangaza mapatano mapya

NEW YORK, Marekani



SERIKALI ya China na Marekani zimeafikiana kutowekeana ushuru mpya wakati nchi hizo zikifanya majadiliano   kufikia makubaliano ndani ya siku 90.

Makubaliano hayo yalifikiwa jana mjini hapa  kati ya Marais Donald Trump na Xi Jinping.

Ikulu   ilieleza kuwa katika makubaliano hayo, Rais Trump alikubali kutopandisha ushuru kwa hadi asilimia 25 kwa bidhaa za China zenye thamani ya dola bilioni 200 ifikapo Januari mosi kama ilivyokuwa imetangazwa   awali, baada ya China kukubali kununua kiwango kisichotajwa lakini muhimu, cha bidhaa za kilimo, nishati, viwandani na nyingine.

Mapatano hayo yaliyofikiwa baada ya   chakula cha usiku kilichodumu kwa zaidi ya  saa mbili, yanatoa muda kwa mataifa hayo mawili kushughulikia tafauti zao katika mzozo unaohusu kampeni ya ushari ya China kuchukua nafasi ya udhibiti wa Marekani wa nyanja ya teknolojia.

“Ni makubaliano ya kushangaza,” Trump aliwaambia waandishi wa habari akiwa  kwenye ndege ya Air Force One.

“Tutakachofanya ni kusimamisha mpango wa kupandisha ushuru. China itazungumza, China itaondokana na ushuru. China itakuwa inanunua bidhaa nyingi kutoka kwetu,” aliongeza Rais Trump.

Ikulu  ilisema pia kwamba China imeacha milango wazi kuweza kuidhinisha makubaliano ambayo  awali hayakuidhinishwa   ikiwa yatalazimika kuwasilishwa tena.

Julai, Qualcomm ambaye ndiye  mtengenezaji mkubwa  duniani wa vifaa vya kuhifadhi kumbukumbu  katika simu za kisasa,  iliachana na mpango wa  dola bilioni 44 wa kununua vipitishi  vya umeme kutoka NXP, baada ya kushindwa kupata idhini ya mamlaka ya udhibiti ya China, na kuwa mwathirika wa ngazi ya juu wa mgogoro wa biashara kati ya China na Marekani.

Ilisema ikiwa makubaliano kuhusu masuala ya biashara, ikiwemo uhamishaji wa teknolojia,  vikwazo visivyo vya kodi, wizi wa mtandaoni na kilimo,  hayajafikiwa na China katika   siku 90, kwamba pande zote mbili zinakubaliana  ushuru wa asilimia 10 utapandishwa  hadi asilimia 25.

Awali, Rais Trump aliweka ushuru wa asilimia  10 kwa bidhaa za thamani ya dola bilioni 200 kutoka China   Septemba mwaka huu na  China ilijibu kwa kuweka ushuru wake.

Trump pia ametishia kuongeza ushuru kwa bidhaa nyingine za China zenye thamani ya dola bilioni 267.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles