24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Mapengo ya kina Lowassa yazibwa CCM

Edward-LowassaNA JANETH MUSHI, ARUSHA

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Arusha, kimefanya uchaguzi wa kuziba nafasi za uongozi wa chama hicho mkoani humo.

Katika uchaguzi huo, Mbunge wa zamani wa Longido, Michael Laizer, amechaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa CCM wa mkoa kwa kura 515.

Mkutano huo pia  umemchagua Mwandishi wa magazeti ya Uhuru na  Mzalendo Mkoa wa Arusha, Shaban  Mdoe  kuwa katibu mwenezi.

Uchaguzi huo mdogo ulifanyika kutokana na kuhama chama kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM mkoani hapa, Onesmo ole Nangole ambaye hivi sasa ni Mbunge wa Longido kwa tiketi ya Chadema.

Mwingine aliyehama ni  aliyekuwa Katibu wa Itikadi  na uenezi, Isack Joseph ambaye  hivi sasa ni  Diwani wa Kata ya Monduli Mjini na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli kwa tiketi ya Chadema.

Mdoe alishinda kwa kura 36 huku mpinzani wake  Veraikunda Urio, akipata kura 12  katika kura zilizorudiwa awamu ya pili.

Katika awamu ya kwanza, ingawa  Mdoe aliongoza lakini hakufikisha nusu ya kura zilizotakiwa.

Akimtangaza Laizer, Msimamizi wa Uchaguzi huo Steven Wasira, ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, alisema   alipata kura 515 kati ya kura 861 zilizopigwa, akifuatiwa na Emanuel  Makongoro aliyepata kura 338 huku kura nane zikiharibika.

Nafasi hiyo ilikuwa na wagombea watatu akiwamo John Pallangyo aliyekuwa mgombea ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana  ambaye alipata kura 154, Laizer kura 409 na Makongoro kura 330 kati ya kura 903 zilizopigwa

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles