30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Magufuli kuongoza mkutano wa EAC Arusha

RAIS Dk. John MagufuliNa Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

RAIS Dk. John Magufuli, amewasili mkoani Arusha ambako pamoja na mambo mengine, ataongoza mkutano wa 17 wa  wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mkutano huo  utafanyika kesho kutwa mjini hapa.

Dk.  Magufuli aliwasili mjini Arusha jana ambako  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), alilakiwa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na Serikali.

Rais Magufuli kwa sasa ndiye Mwenyekiti Jumuiya ya Afrika Mashariki inayojumuisha   Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.

Kabla ya kuongoza kikao hicho, Rais Magufuli anatarajiwa kuwa na mazungumzo ya ana kwa ana na viongozi wakuu wa EAC.

Machi 3  mwaka huu, yeye pamoja na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, wataweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa barabara ya Arusha – Holili – Taveta – Voi inayoziunganisha   Tanzania na Kenya.

Barabara hiyo ni sehemu ya miradi ya Maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki inayotekelezwa na nchi wanachama wa Jumuiya hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles