23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

LULU DIVA: MILELE ILINIPA WAKATI MGUMU

Na JENNIFER ULLEMBO-DAR ES SALAAM

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Lulu Abasi ‘Lulu Diva’, amesema wimbo wake unaoitwa ‘Milele’, ndio uliompa wakati mgumu tangu alipoanza kujihusisha na tasnia ya uimbaji.

Akizungumza hivi karibuni na MTANZANIA, Lulu Diva, alisema ugumu ulianza wakati wa kuandaa wimbo huo, hadi kukamilisha.

Alisema licha ya kuwa wimbo huo ulimtambulisha vema katika tasnia ya muziki hapa nchini, lakini ulimpa changamoto kubwa ambazo zimebaki kama kumbukumbu kwenye maisha yake.

“Wimbo wangu wa Milele ninauheshimu sana, umenitoa na kunitambulisha katika ulimwengu wa muziki, ila ulinipa wakati mgumu sana kuhakikisha unakamilika,” alisema Lulu Diva.

Lulu Diva alisema wimbo huo ambao video yake ilifanyika nchini Afrika Kusini chini ya mtayarishaji Nicholaus, ulimpa nafasi ya kufika nje ya nchi kwa mara ya kwanza.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles