MBUNGE wa Isiman ambaye Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ametoa Power Tiller 15 kwa madiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa ajili ya kuwasaidia kutekeleza shughuli za maendeleo.
Pia ametoa msaada wa mabati 2,000 kwa ajili ya kukamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo hilo, vyote vikiwa na thamani ya Sh milioni 100.4
Akizungumza na waandishi wa habari juzi,Katibu wa mbunge huyo, Thom Malenga alisema Lukuvi amewapa madiwani mashine ikiwa ni sehemu ya kuwawezesha kuleta maendeleo.
Amewataka madiwani kuwatumika wananchi ipasavyo ili kumuunga mkono mbunge kwa kukuza uchumi wa kila kata na kulifanya jimbo la ismani kuwa na maendeleo ya haraka kwa kuwa madiwani wapo karibu na wananchi .
Akizungumzia msaada wa mabati, Malenga alisema lengo la kuunga mkono kazi zilizofanywa na wananchi ya kusimamisha kuta katika miradi ya ujenzi wa shule ,nyumba za walimu na zahanati ambazo zilikuwa zikihitaji bati ili kukamilisha ujenzi wao.
“Mbunge amewaunga mkono wananchi kwa kazi kubwa waliyoifanya ya kusimamisha kuta za vyumba vya madarasa na zahanati na kwa ajili ya kuwaunga mkono ameamua kununulia bati hizi ili iwe rahisi kukamilisha miradi hiyo ili wanachi wetu waweze kupata huduma muhimu kwa uharaka zaidi,”alisema.
Kwa upande wake,Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Iringa Vijijini, Khalfani Hassani alisema madiwani ndiyo wa kwanza kukutana na changamoto kabla ya kuwezeshwa.