23.3 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Lowassa apongeza serikali kupunguza migogoro

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI Mkuu wa zamani,Edward Lowassa amepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali pamoja na taasisi za dini  kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji mkoani Morogoro.

Alisema hayo jana,wakati wa ibaada  maalumu ya shukrani ya Askofu Jacob Mameo Ole Paulo  wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Morogoro ya kutimiza miaka 25 ya ndoa na 25 ya uchungaji.

Ibada iliyofanyika Usharika wa Bungo, Morogoro mjini, iliongozwa na Askofu Mkuu wa KKKT, Askofu Dk. Fredrick Shoo

Lowassa ambaye katika uchaguzi wa mwaka 2015, aligombea urais kupitia muungano wa upinzani kabla ya kurejea CCM mwaka huu, alisema hali ya vurugu kati ya wafugaji na wakulima mkoani humo  sasa ni shwari.

“Zamani ilikuwa ukifungua vyombo vya habari, unasikia migogoro ya wafugaji na wakulima  Morogoro.

“Sasa hali ni shwari, ninawaomba viongozi na waumini wote tuendelee kuuombea mkoa huu uzidi kuwa na Amani na mshikamano”

Alisema  Askofu  Ole Mameo amekuwa kielelezo kizuri cha kujichanganya na watu na kutatua matatizo yao na kwamba ni mfano mwema kwa viongozi wa kanisa na kiserikali pia.

Aliipongeza Serikali ya Mkoa wa Morogoro  kwa kusimamia vyema suala la utunzaji wa mazingira.

“Serikali ya Mkoa wa Morogoro kwa utunzaji mzuri sana wa mazingira.  Hongera sana mkuu wa mkoa, viongozi na watendaji wote,”alisema.

Askofu Dk. Shoo alisema Askofu Mameo amekuwa mstari wa mbele katika usuluhishi wa migogoro ya wakulima na wafugaji  mkoani humo.

“ Amani siku zote, imekuwa kipaumbele katika kazi yake yote,”alisema,

Ibada hiyo, iliudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na kidini mkoani humo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles