24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

INDIA YASHIKA NAFASI YA NNE KIMATAIFA KWA UWEZO WA SILAHA

Waziri Mkuu wa India Narendra Modi amesema majeshi ya nchi yake yamefanikiwa katika jaribio la kombora la kuangushia satelaiti hatua ambayo imeifanya nchi hiyo kuwa miongoni mwa mataifa makubwa yaliyoendelea katika teknolojia ya kijeshi.

Indiani ni nchi ya nne baada ya Marekani, Urusi na China kufanya jaribio kama hilo.

Waziri Mkuu Modi amesema jaribio hilo limeonesha uwezo wa India katika teknolojia ya anga za mbali.

Tangazo hilo la Waziri Mkuu Modi ni hatua nyingine ya kuonesha uwezo wa kijeshi wa India huku zikiwa zimebakia wiki chache kabla ya kufanyika uchaguzi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles