23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Ihefu yaionya Simba

Na VICTORIA GODFREY-DAR ES SALAAM

UONGOZI wa  Klabu ya Ihefu ya Mbeya, umeahidi kuishangaza Simba kwa kupata matokeo chanya licha ya uzoefu mdogo wa kikosi chao.

Ihefu itakuwa mwenyeji wa Simba, katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2020-12, utakaopigwa  Jumapili hii Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

Timu hiyo ni miongoni mwa timu tatu zilizofuzu Ligi Kuu msimu ujao, zikitokea Ligi Daraja la Kwanza. Nyingine ni Dodoma Jiji na Gwambina ya Misungwi mkoani Mwanza.

Akizungumza na MTANZANIA jana kutoka Mbeya, Ofisa  Habari wa klabu hiyo, Peter Andrew, alisema  wamefanya usajili makini wa wachezaji wenye uwezo wa kukabiliana na changamoto ligi,  licha ya kwamba wengi wao hawana uzoefu wa kutosha.

 “Tumejipanga vizuri, ndio maana tumejaribu  kuchanganya  nguvu za wachezaji  waliobaki  katika timu na hata waliocheza Ligi Kuu lakini wana uwezo wa kutumika kwa muda mrefu, hivyo kupata matokeo ya alama tatu tukiwa nyumbani hilo ndilo tunalolitegemea.

 “Tumepanda Ligi Kuu tukiwa tunajua ugumu wake  lakini tuwahakikshie mashabiki wetu,  Ihefu ipo kwa ajili ya kuleta changamoto mpya katika ligi pamoja na kuondoa ufalme  wa baadhi ya timu katika mpira wa Tanzania,”alisema.

Andrew alitaja orodha kamili ya wachezaji wanaounda kikosi chao cha msimu ujao kuwa ni makipa  Andrew Kayuni, Isihaka Josep na Alex Venance, mabeki Mando Mkumbwa , Omary Kindamba, Eliah Salingo, Emanuel Kichiba, Michael Masinda, Geoffrey Rafael, Allen Malele na Wema Sadoki.

Viungo ni Sudi Mlindwa, Samwel Onditi, John Mbise, Willy Mgaya, Daniel  Jeremiah, Abdi Kassimu,  Ennock Jiah, wakati washambuliaji ni Joseph Kinyozi, Omary Mponda, Malulu   Mponda, Cyprian Kipenye, Issa Ally, Geoffrey Kitenga, Paul Luyungu na Jordan John.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles