Miami, Marekani
Siku chache tangu alipoachana na Kanye West, bibiye Kim Kardashian anatajwa kuwa na ukaribu wa kimapenzi na rapa raia wa Colombia.
Hii si mara ya kwanza kwa wawili hao kuhusishwa na uhusiano wa kimapenzi kwani mwanzoni mwa mwaka huu walionekana wakiwa Miami, Marekani.
Hata hivyo, chanzo kilichohojiwa na jarida la Page Six ni kwamba Kardashian na Maluma ni marafiki tu, hivyo hakuna mapenzi kati yao.
Aidha, chanzo kingine kililiambia jarida la E! News kuwa Kardashian yuko tayari kuanzisha uhusiano wa kimapenzi endapo atapata mwanaume sahihi.