24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Dangote kuinunua Arsenal miaka minne ijayo

Aliko Dangote
Aliko Dangote

NEW YORK MAREKANI

TAJIRI namba moja barani Afrika, Aliko Dangote, yupo katika mipango ya kuinunua klabu ya Arsenal ya England  katika kipindi cha miaka minne ijayo.

Kwa mujibu wa orodha ya watu tajiri duniani iliyotolewa Jumatano iliyopita  na televisheni ya Bloomberg ya jijini New York, Dangote ambaye ni raia wa Nigeria utajiri wake una thamani ya dola za Marekani bilioni 10.9.

Siku hiyo tajiri huyo aliweka wazi nia yake ya kuinunua klabu hiyo tangu mwaka uliopita.

Mnigeria huyo alisema anasubiri biashara zake kuimarika pamoja na uwekezaji wake wa ujenzi wa bomba la gesi na kiwanda cha kusafisha mafuta kabla ya kuinunua klabu hiyo.

“Hakuna tatizo la fedha, nitainunua klabu hiyo pengine miaka mitatu au minne,  tatizo  ni kwamba tuna changamoto nyingi ambazo natakiwa kukabiliana nazo kwa sasa lakini baadaye nitaangalia suala la ununuzi huo,” alisema Dangote akiwa katika mahojiano na televisheni ya Bloomberg jijini New York, Marekani.

Dangote ambaye ni shabiki mkubwa wa Arsenal, amepoteza kiasi cha dola bilioni 4.4 mwaka huu kutokana na kushuka kwa thamani ya fedha ya Nigeria.

Utajiri wake mwingi upo katika kiwanda cha saruji kilichopo mjini Lagos.

Endapo tajiri huyo atainunua timu hiyo  atakuwa mtu wa kwanza kutoka Afrika kumiliki timu iliyopo katika Ligi Kuu England.

“Tatizo si kuinunua  klabu ya Arsenal na kuendeleza yaliyopo badala yake ni kufanya mabadiliko ndani ya klabu hiyo.

“Nimekuwa na mafanikio makubwa katika biashara na nafikiri naweza pia kuendesha klabu hiyo kwa mafanikio makubwa,” alisema Dangote.

Klabu ya Arsenal imeshinda ubingwa wa Ligi Kuu England mara 13 huku wakijivunia 2004 kuwa mwaka bora zaidi katika klabu hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles