24 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Cristiano Ronaldo hana tofauti na film ya Revenant

Cristiano Ronaldo
Cristiano Ronaldo

ADAM MKWEPU NA MITANDAO,

MWAKA 2002,  mashabiki wa timu ya Manchester United walihamaki na kudai  kocha wa  zamani wa timu hiyo, Sir Alex Ferguson  hawezi  kuendelea  kuifundisha timu hiyo kwa kuwa hakuwa na jipya.

Mwandishi wa gazeti la Sunday Times la Uingereza,  Hugh Mcllvanney  anasema kwamba baadae mashabiki hao walisikika wakisema kwamba  kocha huyo alikuwa na bahati ya kuendelea na kibarua hicho.

Mcllvanney anaongezea kuwa labda  mashabiki hao walitakiwa kuhakikisha  kocha huyo anazikwa kabla ya kusherekea msiba wake kwa kuwa  Sir Ferguson anaamini anaweza hasife katika kizazi chake.

Huo mstari wa mwisho wa Mcllvanney bado unaendelea kuzivuruga akili za mashabiki hao si kwamba unapatikana katika film ya Leonardo DiCaprio aliyechukuwa tuzo ya mwigizaji bora anayefanana na Brian Kilcline.

Sababu kubwa ni Cristiano Ronaldo amekuwa katika vichwa vyao mithiri ya film ya ‘Revenant’ ndani ya michuano ya Euro 2016.

Katika hatua ya makundi nyota huyo alizidisha mzuka wa Iceland na kitendo chake cha kukosa penalti katika mchezo dhidi ya Austria,kilikosolewa  na kumfanya  afanye mambo  makubwa kuliko  ilivyotarajiwa.

Kulikuwa na maswali machache yasiyostahili yakimaanisha huenda kiwango cha Ronaldo kimekwisha  ingawa ni haki kwa kila binadamu anayefikiri sawasawa.

Ni kweli kwamba mashabiki wa soka hawawezi kunyamaza kuelezea mapungufu wanayoyaona kutoka kwa wachezaji hodari lakini Ronaldo anaamini ataendelea kuishi milele katika vichwa vya kizazi chake baada ya michuano ya Euro 2016.

Kukosolewa na kunyooshewa kidole ni moja ya changamoto zilizomjenga nyota huyo  katika michuano ya Euro 2016 na kuanza kufanya vizuri licha ya awali kuonekana hana bahati.

Ronaldo anaamini  katika ubora wake wa kipekee, ingawa bado anajiuliza kama atakuja kupata nafasi nyingine  ya kushinda michuano mikubwa kama hiyo  akiwa  nahodha wa Ureno.

Kila akifikiria umri wake hana jinsi, kwani akiwa na umri wa miaka 19 alishuhudia timu yake ikifungwa dhidi ya Ugiriki katika fainali ya Euro 2004 na baada ya kukosa nafasi ya kutwaa taji hilo alijikuta akidondosha chozi la uzuni na uchungu kwa  taifa lake.

Tangu hapo amefanikiwa kucheza nusu fainali mbili ikiwamo ya Kombe la Dunia mwaka 2006 na Euro mwaka 2012 kabla fainali ya jana.

Lakini  katika kampeni ya kufuzu kushiriki michuano ya Kombe  la Dunia ndani ya miaka miliwi iliyopita, Ureno ilionekana kupotea katika ulimwengu wa soka Duniani.

Ureno imeingia Euro 2016 ikiwa na mchezaji wa nafasi ya beki mwenye umri wa miaka 38, hiyo ilikuwa ikimaanisha haikuwa na beki wala winga wa  kueleweka huku mfumo  waliokuwa wakicheza ulionekana  kama uyoga  kutokana ulivyokuwa wa kubahatisha.

Timu nzima ilikuwa ikitegemea uwezo wa Ronaldo na ukweli juu ya hilo ulionekana katika mchezo dhidi ya Wales na Hungary.

Ushawishi wa nyota huyo ndiyo uliijenga  timu hiyo, kadri muda ulivyozidi  kuyoyoma kama ilivyotokea kwa Diego Maradona katika  fainali ya Kombe la Dunaia nchini Mexico, mwaka 1986 ambapo alifanikiwa kufunga mabao matatu na kutengeza matatu.

Michuano ya Euro 2016 iliyomalizika jana ilimpa nafasi Ronaldo ya kutengeneza CV kwa hatua aliyofikia kwa kuiongoza vena timu yake ya taifa ya Ureno.

Wakati walipotoka sare ya bao 1-1 katika hatua ya makundi ilifahamika bao dhidi ya Austria lingeweza kuwaondoa kwenye michuano hiyo.

Ureno hawakukata tamaa na kujikuta  wakibadilika kila kitu katika timu yao baada ya kuanza kushinda kwa ushambuliaji wa kushitukiza.

Kusuasua kwao kuliwafanya kujiuliza wakiwa nafasi ya tatu katika kundi lao ambapo safari yao ilianza kuwa hadithi ya kipekee  kwa kuanza kuzifunga Croatia. Poland na Wales.

Kufanikiwa  kwa Ureno na kufanikiwa kwa Ronaldo kutimiza majukumu yake ipasavyo  uwanjani kama nahodha wa timu  hiyo, thamani yake inaweza kupanda na kuwa zaidi ya Lionel Messi na Zinedine Zidan ambaye amekuwa mchezaji bora kuwahi kutoka tangu enzi za Maradona.

Ubora wa Ronaldo unachangiwa na vitu vingi hivyo kwa wanaomchukia  haimaanishi  wataendelea kuwa katika hali hiyo kila wakati, kutokana na mafanikio yake nyota huyo ataendelea kuwa revenant ambayo inaelezea kwamba mtu akifanya makubwa jina lake litaendelea kuishi kutokana na kile ambacho amekifanya.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles