24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Chelsea, West Brom watozwa faini

ChelseaLONDON, ENGLAND

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Chelsea na klabu ya West Brom, wametozwa faini kwa utovu wa nidhamu uwanjani katika mchezo ambao ulipigwa mwezi uliopita zilipokutana timu hizo.

Shirikisho la Soka nchini England (FA), limeitoza Chelsea faini ya pauni 65,000, wakati huo West Brom kwa ikipigwa faini ya pauni 35,000.

Mshambuliaji wa Chelsea ambaye anaonekana kuwa na utovu wa nidhamu, Diego Costa, alihusika katika mambo mengi yaliyoashiria kwamba ni ya utovu wa nidhamu.

Mhispania huyo alishambuliana na kiungo wa kati wa West Brom, Claudio Yacob, baada ya kuangushwa chini.

Katika mchezo huo, West Brom walikuwa ugenini kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, ambapo klabu hiyo ilifanikiwa kutoka sare ya 2-2 dhidi ya wapinzani hao.

Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari, FA inasema kuwa timu zote mbili zilishindwa kudhibiti wachezaji wake.

Hata hivyo, mchezaji ambaye alisukumana na Coasta, Yacob, alioneshwa kadi ya njano na kocha wake, Tony Pulis, aliamua kumtoa nje mchezaji huyo.

Siku chache baadaye kocha wa Chelsea, Guus Hiddink, alielezea kutoridhika na uamuzi wa refarii wa mchezo huo, Anthony Taylor, akisema kuwa alipaswa kumuonesha kadi nyekundu Yacob.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles