LONDON, England
CHAMA cha Soka England (FA) kimempa mkataba mpya wa miaka mitatu kocha wake wa timu ya taifa, Gareth Southgate, hivyo ataendelea na majukumu yake hadi mwaka 2024.
Itakumbukwa kuwa mkataba wake ulitarajiwa kufikia ukomo baada ya tu ya kumalizika kwa fainali za Kombe la Dunia za mwakani huko Qatar.
Mbali ya Southgate, mwingine aliyepewa mkataba mpya ni msaidizi wake, Steve Holland, ikimaanisha watakuwa na kikosi hadi kwenye fainli za Euro za mwaka 2024 zitakazofanyika Ujerumani.
“Nimefurahi kuona mimi na Steve tumeweza kuongezewa mikataba katika majukumu yetu,” amesema Southgate katika taarifa iliyotolewa na FA.