25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

2 CHAINZ, KESHA WARD WAFUNGA NDOA

MIAMI, MAREKANI


RAPA Tauheed Epps, maarufu kwa jina la 2 Chainz, amefanikiwa kufunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu, Kesha Ward, huku mastaa mbalimbali wakijitokeza kwenye sherehe hiyo.

Rapa huyo alikuwa kwenye uhusiana na Kesha kwa muda mrefu, lakini miaka mitatu iliyopita waliamua kuweka wazi kila kitu na kuvishana pete ya uchumba.

“Ninashukuru sana, nimefanikiwa kufanya kile nilichokipanga kwa muda mrefu mjini Miami, kwa sasa nipo kwenye muunganiko na Kesha Ward, tumeweza kuwakutanisha marafiki karibu kwenye hoteli ya Villa Casa Casuarina,” aliandika 2 Chainz.

Baadhi ya mastaa ambao walionekana kwenye sherehe ya harusi hiyo ni pamoja na Kanye West na mke wake, Kim Kardashian, Alicia Keys na mume wake Swizz Beatz pamoja na Gucci Mane.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles