25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

ZITTO ASINGEGOMBANIA HUENDA  ANGEKUWA MZITO

IKIWA ni  takribani miaka  mitatu tangu Zitto Zuberi Kabwe ahame kutoka Chadema  kwenda  ACT,  bado  mijadala haikukoma dhidi yake.

Zitto kuendelea kujadiliwa baada ya kutimkia ACT ni kutokana na  mchango wake katika kuijenga Chadema ambapo baadhi ya  wananchi wanadai kuwa huwezi kuzungumzia nguvu ya chama hicho ukampuuzia  mwanasiasa  huyu ambaye  kutokana na uwezo wake wa kujenga hoja  alisababisha vijana wengi kunogewa  na  mabadiliko.

Mwaka 1992, Zitto akiwa na umri wa miaka 16 alijiunga na Chadema  mara baada ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi  na baadaye mwaka 2005  akiwa na  umri wa miaka 29,   alifanikiwa kuchaguliwa  kwa mara ya kwanza  kuingia bungeni kupitia chama hicho akiwakilisha Jimbo la Kigoma Kaskazini.

Akiwa  bungeni Zitto amekuwa kivutio  kutokana na misimamo yake katika  kutetea maslahi ya umma ikiwamo kupinga ufisadi na  kubadilisha baadhi ya sheria mbovu.

Hata hivyo  mbali na kuipigania Chadema  ndani na nje ya Bunge  bado  Zitto  alifukuzwa   kutokana na kilichotafsiriwa utovu wa nidhamu.

Zitto akihisiwa kuwa kibaraka wa CCM, ili kuuzika upinzani, lakini inasemekana mgogoro   uliompa talaka msomi huyu wa uchumi ni kukimezea mate kiti cha mfalme.

Ni wazi mgogoro huu  uliosababisha  Zitto kutimkia ACT  2015 mwaka ambao kimsingi ulikuwa ni wa Uchaguzi Mkuu,  kwa kiasi fulani ulidhoofisha  upinzani.

Ulidhoofisha upinzani kwa maana ya kwamba pamoja na kuwapo umoja wa Ukawa lakini ikumbukwe  ACT  haikuwamo katika umoja huo.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Dk. Patrick  Asingo wa  Kenya ni kwamba  vyama  vya upinzani Afrika vimekuwa vikishindwa kuviondoa vyama tawala kutokana na kukosa ushirikiano.

Dk. Asingo ameitumia Kenya ambapo vyama vya upinzani kwa kukosa umoja vilishindwa kuiondoa KANU katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1992 na 1997.

Aidha  msomi huyu  kwa kuonesha  nguvu ya umoja ndani ya  upinzani, amevitumia vyama vya  NAK na LDP, vilipojitambua na hatimaye  kuunda umoja wa NARC, mwaka 2002  vilifanikiwa   kuing’oa KANU madarakani.

Dk. Asingo katika utafiti wake ameonesha kuwa  si tu umoja peke yake wa  upinzani hufanikisha  kuondoa  chama tawala,  bali pia na  sababu nyingine kama  Serikali  kulemewa na vitendo vya ufisadi huku pengo la maskini na matajiri likizidi kuongezeka.

Zitto  akingali  Chadema aliwahi  kuhojiwa na  Jamii Forum mwaka 2012 kwamba Je, anaona tofauti ipi ya msingi kati ya CCM na Chadema ambapo  alijibu kwa kusema: ‘‘CCM imeshindwa kupambana na adui ufisadi, Chadema tunapambana na tutapambana na ufisadi kwa nguvu zetu zote.’’

Majibu  ya Zitto yalikuwa sahihi kwani katika miaka ya nyuma   upinzani ulikuwa  ukijiongezea umaarufu kwa kutembelea kete ya ufisadi uliokuwa umeota mizizi ndani ya Chama Cha Mapinduzi.

La kujiuliza kama upinzani unaozidi kugawanyika ulikuwa unazaa matunda kutokana na chama dola kulemewa na ufisadi,  leo hii JPM anaendelea kusifika  kwamba anawapa kichapo mafisadi, Je nini matokeo yake?

Haitoshi Zitto aliwahi kusema kuwa ndani ya Chadema kuna  utaratibu mzuri wa kujieleza hivyo   yeye binafsi, Dk. Slaa, Mbowe na Prof. Mkumbo  ni  Presidential Materials, lakini sasa hivi miongoni mwao  hawako huko, nini hatima yake?

Wakati   Zitto mwenye kuonekana bado anajikongoja  kisiasa akisema katika Uchaguzi Mkuu ujao hagombei  ubunge  bali Urais, pamekuwapo na  tetesi kuwa ACT  inajiunga kinyemela na Ukawa ili kuimarisha upinzani, lakini la kujiuliza ni Je atakubaliwa kupewa uzito ili akawe  mzito Magogoni?

Ndugu Zitto Kabwe

 

,

 

 

 

 

 

 

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles