25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Usher atumia saa 3 kuchora ‘tattoo’

LOS ANGELES, MAREKANI 

MKALI wa muziki wa RnB nchini Marekani, Usher Rymond, ametumia saa tatu kuchora michoro nyuma ya shingo na kichwa chake.

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 40, alikutana na mchoraji maarufu wa michoro jijinu Los Angeles, Dillon Forte na kuchora michoro hiyo ambayo inajulikana kwa jina la geometric patterns (Mifumo ya Kijiometri).

“Nimekuwa nikimsikiliza Usher akiimba tangu nikiwa na umri wa miaka 11, lakini leo ninajisikia kuwa na furaha kupata nafasi ya kufanya naye kazi, jambo la kujivunia kuniamini niweze kumchora mwilini mwake,” aliandika Forte kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Usher amekuwa kimya kwa muda mrefu, mara ya mwisho kuachia wimbo wake mpya ilikuwa Septemba 2016, ambapo aliachia wimbo wa Hard II Love, lakini amekuwa akionekana katika studio huko jijini California, hivyo kuna uwezekano mkubwa wa kuachia wimbo mpya.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles