24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Trump ajitokeza kwa kushtukiza mgahawani New York

92470151_mediaitem92470150
Rais Donald Trump akiwa mgahawani

Rais mteule wa Marekani Donald Trump aliwashangaza wateja, na wanahabari wanaofuatilia safari zake, baada ya kujitokeza kwa kushtukiza katika mgahawa mmoja New York.

Wanahabari waliopewa kazi ya kufuatilia safari zake walibaki kushangaa kwani walikuwa wameelezwa kwamba angesalia nyumbani jioni hiyo.

Lakini badala yake, aliandamana na kundi dogo la maafisa hadi kwenye mgahawa wa 21 Club katika mtaa wa Manhattan, mmoja wa migahawa anayoipenda sana.

Video zilizopigwa wakati wa kisa hicho zinamuonyesha Rais Trump akiwasalimia wateja na kuwaambia kwamba atapunguza kodi wanayolipa kwa serikali.

Hatua ya kutofuata desturi na kutowafahamisha wanahabari wanaomfuatilia rais mteule kuhusu safari hiyo imevitia hofu vyombo vya habari Marekani.

Msemaji wa Trump, Hope Hicks baadaye aliwaambia wanahabari kwamba hakufahamu mipango ya Rais Trump na akawaahidi wanahabari kuwa watapata uhuru wa kufikia maafisa wa serikali na taarifa za serikali kama ilivyokuwa chini ya marais wengine.

Chama cha Waandishi wa Habari wa Ikulu ya White House kimeshutumu kisa hicho. Viongozi wa chama hicho wamesema “haikubaliki kwa rais ajaye wa Marekani kusafiri bila waandishi wa habari wa kufuatilia habari zake na kuwafahamisha wananchi kuhusu alipo”. Source: BBC Swahili

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles