25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Saudi Arabia kuboresha miundombuni Urusi

BUENOS AIRES, Argentina



MKURUGENZI Mkuu Mtendaji wa wa Mfuko wa Uwekezaji  nchini hapa (RDFI),   Kirill Dmitriev amesema  takribani dola bilioni moja kutoka mfuko wa pamoja baina ya nchi hii na Saudi Arabia zitatumika kwa ajili ya kuboresha miundombinu kuanzia mwakani.

Mkurugenzi huyo alitoa taarifa hiyo jana katika alipozungumza na waandishi wa habari akisema tayari wenzao wa Saudi Arabia wamethibitisha nia yao ya kuwekeza katika miradi ya miundombinu nchini hapa.

“Saudi Arabia wameshathibitisha nia yao ya kushiriki katika uwekezaji katika miradi kadhaa ya miundombinu ambayo iliwasilishwa na  RDIF na  miaka mingine ijayo tunapanga kuwekeza dola nyingine bilioni mbili kutoka katika mfuko wa pamoja wa Urusi na Saudi Arabia,”alisema  Dmitriev.

Alifafanua kwamba miradi 12 ilipendekeza na mfuko wake huo na yote itaanza kufanyiwa kazi.

Dmitriev alisema  miongoni mwa mambo yaliyozungumzwa kwenye  mkutano baina ya kiongozi wa nchi hii,  Vladimir Putin na Mfalme wa Saudi Arabia, Prince Mohammed bin Salman   ni kuhusu nchi hiyo kuongeza uwekezaji nchini hapa.

Alisema  matunda ya uwekezaji wa Saudi Arabia nchini humu yameshaanza kuonekana.

“Miaka miwili iliyopita uwekezaji wa Saudi Arabia ulikuwa hauna kitu, lakini sasa umeshazaa zaidi ya dola bilioni mbili,” alisema Dmitriev.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles