24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Sanare aagiza ofisa mapato Morogoro asimamishwe kazi

Na Ashura Kazinja -Morogoro

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Loata ole Sanare ameagiza Ofisa Mapato wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Charles Komba asimamishwe kazi mara moja kutokana na utoro kazini na kutohudhuria kikao cha Baraza la Madiwani kilichotakiwa kufanyika Mei 26, mwaka huu.

Sanare alitoa agizo hilo mwanzoni mwa kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro kilicholenga kujadili taarifa na majibu ya hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19, jana.

Akiendesha kikao hicho, Sanare alitaka kujiridhisha iwapo wakuu wa

idara wote na vitengo wameshiriki kama ilivyokuwa imeelekezwa siku chache kabla ya kikao hicho, ndipo alibaini kutokuwepo ofisa huyo.

Alisema kibali alichokuwa ameomba kusafiri tangu siku ya kikao hicho, kilikuwa hakijapitishwa na

mkurugenzi wa halmashauri, huku akiwa hayupo kazini.

Alipoulizwa mkuu wake wa Idara ya Uhasibu kuhusu kutokuwepo kwake kazini, alikiri mtumishi huyo aliomba ruhusa, hakuruhusiwa na alitaarifiwa asiondoke.

Sanare alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya

ya Morogoro, Rehema Bwasi kumsimamisha kazi mara moja,

huku akimtaka pia kusimamisha mshahara wake hadi pale suala lake

litakapopatiwa ufumbuzi.

“Yaani nikitoka sasa hivi hapa uwe umemwandikia barua ya kumsimamisha kazi huko huko alipo kwa utoro wake, usimlipe mpaka jambo lake litakapopatiwa utatuzi,” alisema Sanare.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles