23.6 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

MSUNGU AGEUKIA GOSPO  

Stanley MsunguNA EDO BRIAN

MSANII wa filamu za Kibongo, Stanley Msungu ameamua kugeukia uimbaji wa muziki wa Injili na tayari ameshaachia wimbo mmoja unaojulikana kwa jina la Nimerudi.

Msungu ambaye pia hujulikana kama Senator ameliambia Swaggaz kuwa, anamshukuru Mungu kwa vipaji anavyompa na yupo tayari kurudi mikononi mwake kumtumia kwa dhati.

“Wengi wanajua mimi ni mwigizaji pekee, lakini pia naishi ndani ya Yesu… na sasa nimeamua kumtumikia Mungu kupitia kipaji changu. Wimbo wa Nimerudi ni mwanzo wa cheche zangu kwenye Gospo,” alisema Msungu ambaye ameshauachia wimbo huo kwenye mtandao wa YouTube.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles