23.6 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Mazungumzo muhimu kuliko viboko

fimbo

NA MANENO SELANYIKA, DAR ES SALAAM

KADIRI dunia inavyobadilika ndivyo malezi ya watoto nayo yanabadilika.

Miaka ya nyuma walezi au wazazi walitumia njia ya kuwachapa viboko watoto kama adhabu pekee inayoweza kumrekebisha mtoto kitabia.

Hivi sasa kada mbalimbali wakiwamo watoto wenyewe wanaona adhabu ya viboko si nzuri kwa madai kuwa inamjengea mtoto woga, usugu na ujeuri.

Akizungumza na TOTO kona mapema wiki hii Rahma Mfaume (10), anayeishi na wazazi wake maeneo ya Kinondoni Msisiri, Dar es Salaam anasema kumpiga mtoto si adhabu sahihi kwa karne hii.

“Ni kweli wakati mwingine sisi watoto tunafanya makosa yanayostahili adhabu lakini, mnafahamu kwamba mkituchapa viboko mnaweza kutusababishia matatizo makubwa kuzidi hayo makosa kama vile visasi, usugu na hata ujeuri,” anasema Rahma

Mtoto huyo anasema ni bora walimu, wazazi na watu wengine wafanye mazungumzo na watoto na si kutumia jazba, vitisho na kuwachapa bakora kwani watawaathiri kisaikolojia.

“Mimi pia nimeshawahi kuadhibiwa na wazazi na walimu shuleni napewa adhabu ya kumwagilia maua au kufanya usafi hii pia ni fundisho kwangu na siwezi tena kurudia kosa lile,” anasema.

Rahma anawaasa watoto wenzake kuacha kiburi pia wasijihusishe na marafiki wabaya watakao waingiza kwenye vishawishi viovu vinavyosababisha wazazi au kuwachapa viboko.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles