25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Majambazi Bunda yaua muuza vitumbua kwa risasi

KALANGI 1Na Ahmed Makongo, Bunda

WAKAZI wa mji wa Bunda mkoani Mara hivi sasa wanaishi maisha ya hofu baada ya kundi la majambazi kuvamia na kumuua muuza vitumbua.

Tukio hilo lilitokea juzi saa 1:40 usiku na kusababisha taharuki kwa wananchi  ambao walilazimika kukimbia   kunusuru uhai wao.

Majambazi hayo yalivamia katika eneo    jirani na Benki ya NMB Tawi la Bunda na kufyatua risasi ambayo ilimuua kijana huyo.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, majambazi hayo pia  yalivamia katika vibanda vya M-pesa vilivyoko katika eneo la kituo cha  zamani cha mabasi mjini Bunda   yakiwa yanarusha risasi ovyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Philip Kalangi, alisema   iliwalazimu askari waliokuwa zamu katika benki ya NMB kujibu mapigo kwa kufyatua risasi.

“Risasi nyingi ni za polisi waliokuwa lindoni pale benki ya NMB waliona wajibu mapigo kwa kufyatua risasi,” alisema Kalangi.

Mmoja wa wafanyabiashara ambao kibanda chake cha M-pesa kilivamiwa na majambazi hayo, Omar Rashid, alisema   watu hao waliokuwa na bunduki walimteka na kumtaka atoe fedha  zote alizokuwanazo.

Alisema  majambazi hayo yalichukua zaidi ya Sh 800,000 zilizokuwa kwenye droo na simu yake ya mkononi ya kutolea huduma ya M-Pesa  iliyokuwa na zaidi ya Sh milioni moja.

“Ilikuwa kama saa moja na dakika 45 hivi nilishutukia wanapiga risasi, nikiwa bado ninashangaa wakavamia katika kibanda changu wakitaka niwape fedha zote nilizokuwa nazo.

“Kabla sijatoa tu mmoja alikuwa na kama nyundo akataka kunipiga nikatoa droo ya fedha nikawapa na wakachukua na simu yangu ya M-Pesa,” alisema Rashid.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles