25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

TANZANIA YAONGOZA KWA MARADHI YA KIPINDUPINDU

Shirika la Afya Duniani (WHO), imeitaja Tanzania kuwa  miongoni mwa nchi 10 kinara kwa watu wake kuugua ugonjwa wa kipindupindu.

Mataifa  mengine yaliyotajwa ni pamoja na India ambayo ndiyo inayoongoza. Nyingine ni Haiti, Jamhuri  ya  Kidemokrasi  ya  Congo, Tanzania, Bangladesh, Uganda,  Msumbiji na Kenya, ambayo ilikumbwa na mlipuko mkubwa wa maradhi hayo kwa nyakati tofauti mwaka huu.

Katika ripoti yao iliyotolewa hivi majuzi, imesema kuwa sababu kuu ya kuandamwa na maradhi hayo ni kukithiri kwa mazingira machafu katika mataifa hayo.

Ripoti hiyo inasema kuwa watu bilioni 1.2 sawa na moja ya sita ya watu wote duniani wako hatarini kukumbana na maradhi hayo hatari.

Wakati Bara la Afrika likikumbwa na kadhia hiyo kutokana na unywaji wa maji yasiyofaa, hali ni tofauti kwa  Ulaya na Amerika ya Kaskazini ambako mifumo imara ya maji taka imeyafanya mabara hayo yawe huru na kipindipindu kwa miongo mingi sasa.

Lakini watu zaidi ya bilioni mbili wamebakia bila maji safi na mifumo ya maji taka, hivyo, kipindupindu kinaendelea bila huruma kuathiri watu masikini zaidi duniani na ndani ya kila nchi athirika.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles