23.6 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Taarifa za mfumo wa anwani za makazi kutumika kwenye mawasiliano

Na Mwandishi Wetu, Pwani

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, Kaspar Mmuya ameshauri Watendaji kuanza kutumia taarifa za mfumo wa Anwani za makazi Postikodi kwenye barua za ofisi ili kurahisha mawasiliano kwa watu kujua eneo zinapopatikana Ofisi.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, Kaspar Mmuya akizungumza na Watendaji (hawapo pichani) katika Ofisi ya Mtendaji, Kata Matumbi kukagua utekelezaji wa operesheni ya Anwani za makazi Halmashauri ya Mji wa Kibaha.

Naibu Katibu Mkuu huyo ameyasma hayo leo Alhamisi Mei 19, 2022 katika ziara yake ya kikazi katika Halmashauri ya Kibaha Mji, mkoani Pwani alipofika kujionea utekelezaji wa Operesheni Anwani za makazi.

“Watendaji tuanze kujitambulisha kwenye mikutano kwa mfumo wa Anwani za makazi ili kutoa hamasa zaidi kwa wananchi,” amesema Mmuya.

Upande wake Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Mkoani A Kibaha, Jakson Mwakalima amesema tayari wameshapata mtengenezaji wa vibao vya nyumba, ambavyo mwananchi anaenda kununua kwa shilingi elfu Mbili na kubandika kwenye nyumba yake.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu, Kaspar Mmuya akitoa maelekezo kwa Watendaji wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Mji, mara baada ya kukagua utekelezaji wa Operesheni Anwani za Makazi katika Halmashauri ya Mji huo.
 
- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles