24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

RC Mtwara: Sheria ya Sospa ilitungwa kwa mihemko ya wanaharakati

Nora Damian, Mtwara



Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Glasius Byakanwa, amesema Sospa ilitungwa kwa jazba na mihemko ya wanaharakati kwa sababu haimfanyi mtoto wa kike awajibike.

Aidha, amesema suala la mimba za utotoni bado ni changamoto kubwa mkoani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi Novemba 18, amesema changamoto hiyo kwa kiasi kikubwa inachangiwa na udhaifu uliopo katika Sheria ya Makosa ya Kujamiiana (Sospa 1998) ambayo amedai haimfanyi mtoto wa kike awajibike.

“Sospa ilitungwa kwa jazba na mihemko ya wanaharakati. Najua wanaharakati wa jinsia wanaweza wakachukia lakini mimi ni baba wa watoto wa kike pia nataka watoto wa kike wawe responsible (wawajibike),” amesema Byakanwa.

Amesema suala la mimba za utotoni linahitaji tafakari kubwa na kwamba kuendelea kumuadhibu mwanamume kutamfanya mtoto wa kike asiwajibike kwa kujizuia.

“Unamfunga mwanamume miaka 30 maana yake unaruhusu mtoto atakayezaliwa akue hana mzazi,” amesema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles