27.2 C
Dar es Salaam
Monday, May 6, 2024

Contact us: [email protected]

PUTIN, TRUMP KUKUTANA KUHUSU SYRIA

MOSCOW, URUSI


WAZIRI wa Habari wa Urusi, Dmitry Peskov amesema Rais Vladimir Putin wa hapa na Rais Donald Tump wa Marekani wataujadiliana kwa kina mgogoro wa Syria wakapokutana baadae mwezi  huu.

Viongozi hao wawili wanatarajia  kukutana mwezi huu wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Maendeleo Asia na Pasifiki (APEC) utakaofanyika nchini Vietnam.

Kwa sasa Rais Trump yupo katika ziara ndefu  ya kikazi katika nchi za Asia na Pasifiki.

Akizungumza  na waandishi wa habari jana mjini Moscow, waziri alisema katika majadiliano ya marais hao kutakuwapo na ajenda nyingi lakini kubwa itakuwa ni kuhusu mgogoro wa Syria watakaoupangia muda zaidi ili kuupatia ufumbuzi.

Alisema kwa sasa kuna mafanikio mengi  kuhusu kutatua mgogoro huo wa  Syria,lakini kunahitajika ushirikiano mpya ili kuhakikisha amani inarejea katika maeneo ambayo yalikuwa  yanakaliwa na magaidi wa kimataifa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles