25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Polisi haijakamilisha upelelezi wafanyakazi Kituo cha Sheria

4c36Suleiman-KovaAsifiwe George na Jenipher Thomas(DSJ), Dar es Salaam

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya  Dar es Salaam, limesema linaendelea na upelelezi  wa wafanyakazi na viongozi  38 wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC).

Watu hao wanadaiwa kusambaza taarifa za matokeo ya uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani kabla ya Tume  ya  Taifa ya Uchaguzi (NEC) haijayatangaza.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam,   Suleimani Kova, alisema  watu hao  wanatuhumiwa kukusanya na kusambaza taarifa za uongo katika mitandao ya  jamii  Novemba  9 na 10 mwaka huu.

Alidai  watuhumiwa hao wanatuhumiwa  kuingilia majukumu ya (NEC)   kwamba wakati   matokeo ya kura za uchaguzi mkuu wa 2015 yalikuwa yakisubiriwa,  wao walikuwa wakisambaza taarifa za matokeo kupitia mitandao ya  jamii.

Kova alidai  vijana hao walikiuka maadili ya uangalizi  wa uchaguzi  na kutangaza  matokeo kabla ya NEC  kuyatangaza.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles