25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Peter Banda asaini miaka mitatu Msimbazi

Na Wandishi Wetu

Simba imeanza kuliamsha baada ya leo kumsainisha mkataba wa miaka mitatu mchezaji aliyekuwa anasubiriwa kwa hamu na Wanamsimbazi, Peter Banda raia wa Malawi kutoka timu ya Big Bullet.

Banda anacheza nafasi ya kiungo, lakini ana uwezo wa kumudu sehemu nyingine ikiwamo ushambulaji.

Nyota huyo anakuwa wa kwanza kusajiliwa na Simba kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2021/22.

Kwa mujibu wa taarifa ya klabu ya Simba, wamepanga usajili wa kisayansi ili kuboresha kikosi huku dhamira ya kwanza ikiwa ni kutetea ubingwa pamoja na kufanya vizuri kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles