23.6 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Mwakifwamba atoa onyo kali kwa wasanii

mwakiNA GEORGE KAYALA
RAIS wa Shirikisho la Filamu nchini (TAFF), Simon Mwakifwamba, amewaonya wasanii wa filamu na wale wanaounga mkono Shirikisho hilo kutogombana na amewataka waungane kwa ajili ya kufanya kazi.

Akizungumza na MTANZANIA, Mwakifwamba alisema kuwa kwa muda mrefu kumekuwa na hali ya vuta nikuvute baina ya makundi hayo ya wasanii ugomvi uliochangia kuirudisha nyuma tasnia hiyo

“Tunashukuru ugomvi umeisha, sioni sababu ya wasanii kurudia hiyo tabia ya kutupiana vijembe kwani hatujengi bali tunabomoa hivyo basi adhabu kali itatolewa kwa yeyote atakayeibua ugomvi tena,” alisema Mwakifwamba.

Aliongeza mara baada ya ugomvi huo kumalizika, TAFF wana mpango wa kuunda umoja wa wasanii wote ili uwasaidie kufanya kazi zitakazoifikisha mbali tasnia hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles