25.2 C
Dar es Salaam
Friday, May 10, 2024

Contact us: [email protected]

Mhagama awapongeza watoto walioweka rekodi GGML KiliChallenge

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Jenista Mhagama amewapongeza watoto, Abel Mussa na Rebbeca Damian wenye umri wa miaka 14 waliopanda mlima Kilimanjaro kupitia kampeni ya GGML KiliChallenge – 2023, huku watoto hao wakibainisha kuwa hatua yao hiyo ililennga kuunga mkono jitohada za  Rais Samia Suluhu Hassan hususani katika kuwajali watoto nchini.

Watoto hao wanaolelewa na Kituo cha Moyo wa Huruma kilichoazishwa na kufadhiliwa na Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML), walikuwa ni moja ya washiriki 61 waliopanda mlima Kilimanjaro Julai 14, 2023 na kushuka Julai 20, mwaka huu.

Washiriki hao walipanda mlima huo kupitia kampeni ya GGML KiliChallenge inayolenga kukusanya fedha za kuendeleza mapambano dhidi ya VVU/ Ukimwi.

Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya mashujaa Julai 25, 2023 jijini Dodoma, Mhagama alisema watoto hao walimuambia wamepanda mlima huo kwa kuzingatia kazi kubwa anayofanya Rais Samia Suluhu Hassan ya ulinzi wa watoto wa kitanzani, haki zao na ustawi wao.

“Vilevile kwa kazi kubwa iliyofanywa na Serikali katika ujenzi wa miundombinu ya elimu ya msingi na sekondari na vyuo vikuu. Lakini pia wamesema walipanda kwa kuzingatia kazi kubwa unayofanya kwenye miundombinu ya afya haya yote yakiwa na ustawi mkubwa wa watoto wote wa Tanzania,” alisema.

Amesema mbali na kushirikiana na serikali kusaidia mapambano dhidi ya tatizo la Ukimwi, pia watoto hao ambao ni wanafunzi wa darasa la saba, walipanda mlima huo kwa lengo la kuanzisha moyo wa uzalendo kwa watoto wengine ili watambue kuwa nchi sasa inaoongozwa na rais ambaye anajali ustawi wa watoto.

Kati ya watoto hao, Rebecca Damiani ambaye ni mwanafunzi katika Shule ya Msingi Kivukoni- Geita, alifika katika kilele cha Uhuru cha mlima huo, huku Abel Mussa ambaye ni mwanafunzi wa shule ya msingi Mbugani pia kutoka mkoani Geita, alirudia njiani baada ya kuugua malaria.

Kampeni hiyo iliyoasisiwa na GGML mwaka 2002 kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), mwaka huu ilishirikisha wapanda mlima 35 na waendesha baiskeli 26 waliouzunguka mlima Kilimanjaro kwa siku saba.

Akiwapokea washiriki hao, Julai 20, mwaka huu, Mhagama alimwagiza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuhakikisha wanafunzi hao wanaingizwa kwenye orodha ya miongoni mwa watu watakaohudhuria sikukuu ya mashujaa ambayo imefanyika juzi tarehe 25 Julai 2023.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles