24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Mbunge Segerea akiri hakuna ushirikiano mzuri taasisi za Serikali

Neema Paul ,TUDARCo 

Mbunge wa jimbo la Segerea, Bonnah Kamoli, amesema  kuna ushirikiano mdogo  jimboni kwake kwa baadhi ya taasisi za Serikali kama vile  DAWASA,TANESCO na TARURA katika ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo hususani barabara  hivyo kusababisha uharibifu.

Bonnah ameyasema hayo jana wakati wa ziara yake ambapo ametembelea Kata ya Mnyamani na Kimanga, huku akiandika barua  inayoelezea changamoto hiyo kwa kudai kuwa mawasiliano hafifu baina ya taasisi hizo tatu za serikali ndio sababu ya tatizo.

“Watu wa TARURA wanajenga barabara lakini wakimaliza tu kujenga wanakuja watu wa DAWASA nao wanachimba wanaweka mabomba ya maji sasa hii si sawa,” amesema.

Aidha ametoa wito kwa taasisi hizo kushirikiana wakati wa ufanyaji kazi ili kuepusha uharibifu wa rasilimali na pesa unaotokea kipindi  zinapokinzana katika ufanyaji kazi.

“Unapotokea  ujenzi wowote naomba watu wa DAWASA, TARURA na TANESCO ili washirikiane na kuepusha uharibifu hii itawezekana kama tu kutakua na mawasiliano imara,” ameeleza Bonnah.

Mbunge huyo amezungumzia pia  changamoto ya uhaba wa maji  iliyopo katika jimbo lake kwa muda mrefu kwa kusema kuwa serikali kupitia DAWASA inajitahidi kwa kila hali kuondoa na kubadilisha mabomba ya zamani na kuweka mapya ya sasa hivi.

“Tatizo hili la miundombinu mibovu ya maji wanalijua,wanalishughulikia na wapo mbioni kulimaliza hivyo naomba msiwe na mashaka yoyote,” amesema Bonnah. 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles