28.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, March 19, 2024

Contact us: [email protected]

Marekani yazingirwa na virusi wakati ikisherehekea uhuru

Na MASHIRIKA YA HABARI YA KIMATAIFA

REKODI  mpya ya idadi ya virusi vya corona imeweka wingu mwanzoni mwa  sherehe za uhuru nchini Marekani wakati ongezeko la  maambukizi lailazimisha Uingereza kuwaweka wasafiri kutoka Marekani kwenye orodha mbaya.

Wakati fukwe zimefungwa  kutoka  eneo  moja  la  pwani  hadi  jingine  na  maofisa wakiwataka  Wamarekani  kubakia  majumbani  mwao, hali isiyokuwa  ya  furaha  kuelekea katika  kile  ambacho  kwa  kawaida  ni  mwishoni  mwa  juma kunakochomwa  nyama  na hali  ya  hewa ya  jua  imelemea  mapambano  ya  kudhibiti ugonjwa  wa  COVID-19  katika kitovu  cha  janga  hilo  duniani.

“Ni idadi  usiyoweza  kuamini,”  amesema  Faisal Masud , mkurugenzi wa  matibabu  katika hospitali  ya  Methodist mjini  Texas, ambayo  maofisa  wamesema  inakaribia  kabisa kuzidiwa  na  wagonjwa.

Ukigusa  karibu  kila  nchi  duniani  tangu  kujitokeza kwa ugonjwa huo  nchini  China  mwishoni  mwa  mwaka jana, virusi  vya  corona  vimewaambukiza  kiasi  ya  watu  milioni  10.9  na  kuwauwa  watu 522,000 duniani, na  kuzima  uchumi  uliokuwa  hapo  kabla  ukikua  kwa  kasi na kusababisha  maisha  ya  watu  kuzimika.

Lakini  wakati  Ulaya  na  sehemu  nyingi  za  Asia  kwa  kiasi  kikubwa  zimeweza  kudhibiti virusi  hivyo  vya  corona , kwa upande wake Uingereza  inajitayarisha  kufungua  biashara zake, migahawa  na  kumbi za sinema,  lakini  nchini  Marekani  ugonjwa  huo  umewauwa  karibu  watu 130,000 huku  kukiwa  na  ongezeko  kubwa  la  kesi  mpya  za  maambukizi  ambapo mtaalamu  wa  ngazi  ya  juu  wa  magonjwa  ya  kuambukiza 

Anthony Fauci  amesema; “unaiweka  nchi  nzima  katika  hatari.”

REKODI YA MAAMBUKIZI

Nchi  hiyo yenye  uchumi  mkubwa  duniani  imevunja  rekodi  yake  ya  maambukizi  mapya kwa  siku  ya  tatu mfululizo  hadi  Ijumaa wiki hiii, kwa  kuwa  na  zaidi  ya  maambukizi 57,000 katika  muda  wa  masaa  24. 

Inatarajiwa  kufikisha  maambukizi milioni  tatu  wiki  ijayo, ambapo  kesi  zinaongezeka hususan  upande  wa  kusini  na  magharibi.

Rais  wa  Marekani Donald Trump , akiwa  katika  eneo  la Mount Rushmore kwa  ajili  ya sherehe  za  kurusha  fashifashi pamoja  na  maelfu ya  wahudhuriaji  wakikaribiana  na barakoa  si  lazima, hadi  sasa  amepuuzia  ongezeko  hilo  la  maambukizi  mapya.

Lakini  mtangulizi  wake Barack Obama  amewataka  Wamarekani  kujiweka  “salama  na kuwa  wajanja.”

Sura za Marais wa zamani wa Marekani zilizochongwa katika Mlima Black South Dakota

“Itatulazimu  kuchukua  hatua  kwa  pamoja  kudhibiti virusi  hivi. kwa  hiyo  vaa barakoa. Safisha  mikono  yako. Na wasikilize wataalamu , sio  watu  ambao  wanajaribu  kutugawa,” aliandika  katika  ukurasa  wa  Twitter.

Shirika  la  afya  ulimwenguni WHO limezitaka  nchi  ambazo  zimeathirika  kwa  kiasi kikubwa, “kuamka” na kuona  hali  halisi.

“Watu  wanapaswa  kuamka. Data  hazidanganyi,” Mkurugenzi  wa  masuala  ya  dharura  wa WHO Michael Ryan  aliwaambia  waandishi  habari  mjini  Geneva.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
584,000SubscribersSubscribe

Latest Articles