24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Majambazi waua Mchina, wajeruhi, wapora mamilioni

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Augustino Senga
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Augustino Senga

Na JUDITH NYANGE, MWANZA

MFANYABIASHARA   raia wa China, Maihaimiyan Mai (33) mkazi wa mtaa wa Mahina Kata ya Mhandu wilayani ya Nyamagana   ameuawa kwa kupigwa risasi kifuani nyumbani kwake na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi ambao pia walijeruhi watu wengine watatu na kupora Sh milioni 1.1.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Augustino Senga, alisema tukio hilo lilitokea  Novemba 27, mwaka huu   usiku    wakati Mai akitoka kwenye shughuli zake za biashara.

Alisema wakati Mai alipokuwa akiingia kwenye lango la nyumbani kwake alikutana na watu watatu waliovamia nyumbani kwake huku mmoja kati yao alionekana kuwa  na silaha ambaye alifyatua risasi moja iliyompiga kifuani na kufariki dunia papo hapo.

“Majambazi hao walimshambulia kwa kumpiga na  rungu sehemu mbalimbali za mwili,     Ayoni Mai (29) ambaye ni mdogo wa marehemu,     pamoja na mke wake Christina Kinyonge na   kuwapora   Sh miloni 1.1 na simu mbili za mkononi.

“Pia  walimjeruhi mlinzi wa nyumba hiyo aliyejulikana kwa jina moja la Pascal (35)  kwa kumpiga risasi iliyomparaza kisogoni wakati akitaka kuruka ukuta na kukimbia.

“Majeruhi wote watatu wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando wakiendelea kupatiwa matibabu na mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo  kwa ajili ya uchunguzi, ” alisema Senga.

Senga alisema jeshi la polisi linawasaka watuhumiwa wote waliohusika katika tukio hilo.

Aliwataka  wakazi wa Mkoa wa Mwanza   kutoa ushirikiano kwa jeshi la hilo kuhusu  taarifa za wahalifu hao   waweze kuwakamata na kufikishwa katika vyombo   husika kwa hatua za sheria.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles