28.2 C
Dar es Salaam
Thursday, May 9, 2024

Contact us: [email protected]

Lugalo Gofu yaanza kibabe Mufindi Open 2023

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Wachezaji wa Gofu watakaowakilisha JWTZ katika mashindano ya dunia nchini Marekani wameanza vyema shindano la “Mufindi Southern Highlands Open 2023” linalofanyika Mufindi, Iringa.

Katika shindano hilo, mchezaji Marius Kajuna ameongoza kwa wanaume baada ya kupiga mikwaju ya jumla 69 akifuatiwa na Noel Mheni wote wa Lugalo kwa mikwaju ya jumla 70.

Kwa Upande wa wanawake mchezaji Khadija Selemani amepiga mikwaju ya jumla 74 akifiatiwa na Leticia Kapalia kwa mikwaju 78 wote wa Lugalo.

Ofisa Habari wa Klabu ya Gofu Lugalo, Meja Selemani Semunyu amesema shindano la “Mufindi Southern Highlands Open 2023” ni muendelezo wa maandalizi kuelekea kwenye Shindano la Dunia la Majeshi (CISM) huko San Diego, Marekani Oktoba, 2023.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles