27.2 C
Dar es Salaam
Thursday, May 2, 2024

Contact us: [email protected]

JPM: TUNALIPA DENI LA BIL 650/- KILA MWEZI

NA FRANCIS GODWIN, IRINGA


RAIS Dk. John Magufuli amesema Serikali yake imeanza kulipa Sh bilioni 650 za madeni yake kila mwezi.

Hayo aliyasema jana alipokuwa   akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Ndolela, Wilaya ya Iringa wakati akifungua barabara iliyojengwa kwa kiwango cha lami ya Iringa-Migori-Fufu yenye urefu wa kilomita 189.

Alisema madeni hayo ni yale yaliyokopwa na  Serikali  za awamu  zote.

“Tumeanza kulipa madeni haya, kila mwezi tutatoa Sh bilioni 650…madeni haya yalikopwa na awamu zote zilizopita, inawezekana  deni langu  ninalokopa sasa likalipwa  wakati mimi sipo duniani,” alisema Rais Dk. Magufuli.

Alisema deni linalokopwa sasa  linaweza kulipwa hata miaka 50 ijayo kwa sababu linafuata taratibu zilizopo.

“Pamoja na kazi nzuri hii, unaweza  kukutana na mtu anasimama bungeni,  tena anatoka huku huku Iringa akipita  katika barabara hii, alafu anahoji  mbona Serikali inakusanya fedha  nyingi zinakwenda wapi, jambo hili linashangaza,” alisema.

Kutokana na hali hiyo, aliwataka  Watanzania  kutambua uchumi wa  nchi unazidi kukua ukilinganisha na  nchi nyingine za Afrika, kwani umefikia  asilimia saba na bado  unaendelea kukua.

“Serikali ninayoiongoza ina lengo kubwa la kuwasaidia wananchi ambao ni masikini, tutahakikisha wananchi wananufaika na rasilimali zilizopo  bila kubughudhiwa,” aliongeza.

Katika hatua nyingine, Rais Dk. Magufuli alisema sasa ni zamu ya Mkoa wa Iringa kujengewa  miundombinu mizuri kama ilivyo Kanda ya Kaskazini ili Hifadhi ya  Taifa ya Ruaha ipate watalii wengi.

Alisema hifadhi hiyo ina wanyama wa aina zote na  wengi kuliko  hifadhi  nyingine, ila imekosa watalii wengi  kutokana na  kukosekana kwa miundombinu mizuri.

“Tumejipanga kujenga uwanja  wa   ndege wa Nduli kwa kiwango cha lami ili ndege  kubwa ziweze kutua,” alisema.

Rais Dk. Magufuli aliongeza kwamba, ujenzi wa uwanja huo na barabara ya kiwango cha lami kutoka Iringa Mjini kwenda Hifadhi ya Ruaha, kutaongeza watalii zaidi.

Alisema kukamilika kwa barabara   hiyo iliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika na Serikali ya Japan kwa kutoa mikopo yenye riba nafuu, kutawezesha   ukuaji wa uchumi zaidi kwani barabara hiyo kutoka Afrika Kusini  hadi Cairo nchini Misri, ilikuwa haijakamilika upande wa Tanzania  pekee.

“Barabara hii ilikuwa na changamoto kubwa, wasafiri walikuwa wanatumia saa nyingi kufika Dodoma ama mikoa ya jirani, sasa wanatumia saa mbili na kidogo, tuitunze ili iwanufaishe  wananchi,” alisema.

Kwa habari zaidi jipatie nakala ya gazeti la MTANZANIA.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles