24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Filamu ya Tanzania kuonyeshwa Tamasha la Marekani

Aisha filmNA FESTO POLEA

BAADA ya mafanikio makubwa iliyopata filamu ya ‘Aisha’ ilipoonyeshwa kumbi mbalimbali ikiwemo Nafasi Artspace na Pangani, filamu hiyo imechaguliwa kwa ajili ya kuonyeshwa katika tamasha la kimataifa la filamu la New African Films litakalofanyika Washington D.C. nchini Marekani, mwaka huu.

Pia filamu hiyo imechaguliwa kuonyeshwa katika tamasha la kimataifa la filamu duniani katika maeneo manne mashuhuri ambayo ni Los Angeles, Toronto, New York na Singapore.

Ratiba ya maonyesho hayo kwa filamu hiyo ni kama ifuatavyo, Toronto, Canada itaonyeshwa Septemba 23 hadi 29, Singapore itaonyeshwa Septemba 30 hadi Oktoba 6, Los Angeles, Marekani itaonyeshwa Oktoba 14 hadi 20 na New York, Marekani itaonyeshwa Oktoba 21 hadi 28.

Filamu hiyo pia imeendelea kupata neema baada ya kuchaguliwa katika tamasha la kimataifa la filamu la ‘Seattle’ ambalo litakuwa likiadhimisha miaka yake 42 tangu kuanzishwa kwake.

Tamasha hilo litafanyika Mei19 hadi Juni 12, ni tamasha kubwa linalohudhuriwa na watu wengi nchini Marekani ambapo filamu takribani 400 kutoka nchi 80 zitaonyeshwa katika tamasha hilo linalodaiwa kuwa kubwa zaidi Amerika Kusini.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles