23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Amber Rose amjibu Kanye West

amber-rosNEW YORK, MAREKANI

 MWANAMITINDO maarufu nchini Marekani, Amber Rose, amemjibu mkali wa muziki wa hip hop, Kanye West, baada ya kumshambulia msanii, Wizkhalifa.

Wiki iliyopita, Kanye alisema kwamba, Wizkhalifa hasingeweza kutoka na mrembo huyo na kupata mtoto kama hasingeachana naye.

Awali, Kanye alikuwa anatoka na Amber, lakini baada ya kuachana mrembo huyo aliamua kutoka na Wizkhalifa na kusababisha bifu zito kwa wasanii hao.

“Kanye ni mjinga sana, inakuaje anagombana na Wizkhalifa alafu ana mtaja mtoto wangu? Najua yeye ana watoto lakini sijawahi kuwazungumzia hata siku moja lakini yeye sijui ana lengo gani na mwanangu,” alisema Amber.

Hata hivyo, Wizkhalifa hadi sasa hajajibu lolote kutokana na kauli ambayo aliiongea msanii huyo ambaye kwa sasa mke wake ni Kim Kardashian.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles