25.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Adhabu ya Whozu, Billnass, Mboso yabadilika

Na Winfrida Mtoi, Mtanzania Digital

WASANII wa Bongo Fleva, Whozu, Billnass na Mbosso, wametakiwa kulipa faini ili kuruhusiwa kufanya kazi za sanaa nchini kwa kufuata maadili ya Kitanzania.

Uamuzi huo umefikiwa leo Novemba 14,2023 katika kikao cha kusikiliza rufaa ya wasanii hao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Uwanja wa Benjamini Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Awali Whozu alipewa adhabu ya kufungiwa miezi sita kutojihusisha na sanaa na kulipa faini sh. 3 milioni, huku Bilnass na Mboso miezi mitatu kila mmoja.

Baada ya kikao hicho na adhabu ya kufungiwa kuondolewa, Whozu anatakiwa kulipa faini ya sh. 5 milioni, Mboso sh. 3 milioni  na Billnass milioni moja kabla ya kuendelea na kazi zao.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro akimkabidhi Msanii  Whozu mwongozo wa maadili katika kazi za sanaa.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Damas Ndumbaro na Naibu wake Hamis Mwinjuma na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Gerson Msigwa.

Kwa mujibu wa taarifa ya Baraza la Sanaa la Taifa BASATA, msanii Whozu amepewa saa sita ili kutekeleza azimio la kushusha wimbo  wake wa  Ameyatimba kwenye “digital platforms” zote kama makubaliano yanavyoelekeza.

Aidha Waziri Ndumaro amewaasa wasanii hao na wengine nchini kutumia ubunifu kwa kufuata taratibu ulioainishwa katika mwongozo wa uzingatiaji maadili katika kazi za sanaa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles