25.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, May 7, 2024

Contact us: [email protected]

Marekani yafungua mipaka Mexico, Canada

NEW YORK, Marekani

MAREKANI imefungua mipaka yake inayoiunganisha na Mexico na Canada, hivyo raia waliopata chanjo ya Corona kutoka nchi mbili hizo wataingia na kutoka kuanzia Novemba, mwaka huu.

Inafahamika kuwa Marekani iliacha kupokea wasafiri wanaotumia ardhi na vivuko kutoka Mexico na Canada tangu Machi, mwaka jana, sababu kubwa ikiwa ni kuzuia kasi ya maambukizi ya virusi vya ugonjwa huo.

Hata hivyo, bado Marekani imeendelea kuwawekea ngumu wasafiri wasio raia wa Marekani wanaotokea Uingereza, China, India, Afrika Kusini, Iran, na Brazil.

Wiki iliyopita, Kituo cha Kuzuia na Kukabiliana na Magonjwa nchini Marekani ilieleza kuwa wasafiri wote wanaoingia lazima wawe wamepata chanjo ya Corona inayotambuliwa na Shirika la Afya la Kimataifa (WHO) na Taasisi yake ya Udhibiti wa Chakula na Dawa (FDA).

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles