24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Trump, familia yake wachunguzwa kukwepa kodi

New York, Marekani

Maofisa nchini Marekani katika Jimbo la New York, wamesema wamelazimika kuchunguza madai kwamba Rais Donald Trump, amesaidia familia yake kukwepa kodi ya mamilioni ya Dola mwaka 1990.

Rais Trump, amemshutumiwa kwa kuhusika na mpango wa ubabaishaji pamoja na udanganyifu wa ulipaji kodi ili kuficha makadirio yanayomhusu yeye, ndugu na wazazi wake.

hata hivyo, Ikulu ya White House, imetupilia mbali madai hayo kuwa ni ya upotoshaji.

Msemaji wa White House Sara Sanders, ameongeza kusema malipo yote yalikuwa yakikaguliwa na kupitishwa na mamlaka za kodi kwa miaka mingi iliyopita.

Rais Trump, bado hajasema lolote kuhusu madai hayo lakini mwanasheria wake Charles Harder amekana vikali mteja wake kutenda kosa lolote.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles