23.3 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

SERENGETI KUVAANA NA RWANDA LEO

NA MWANDISHI WETU


TIMU ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’, leo inatarajiwa kucheza na Rwanda katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Afrika kwa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa Afcon U-17).

Mchezo huo utakuwa wa tatu kwa Serengeti Boys kucheza katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mchezo wa kwanza uliochezwa Agosti 17, mwaka huu, Serengeti Boys waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Burundi.

Timu hiyo ilipata ushindi mwingine wa mabao 5-0 Sudan, katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Fainali za Afcon U-17 inatarajiwa kuchezwa mwakani nchini, ambapo timu itakayoibuka mabingwa katika michuano ya  Cecafa, itaungana na Serengeti Boys ambayo imefuzu moja kwa moja.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles