23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Putin aazimisha miaka 66 ya kuzaliwa kwake bila sherehe

MOSCOW, Urusi

RAIS wa Urusi, Vladimir Putin jana aliadhimisha siku ya kutimiza miaka  66  ya kuzaliwa kwake ambapo aliitumia kupumzika karibu na ndugu wa familia, marafiki na wasaidizi wake.

Taarifa iliyotolewa jana na msemaji wa Ikulu ya  hapa,  Dmitry Peskov   wakati wa mahojiano na Shirika la Habari la nchi hii, TASS tofauti na walivyo viongozi wengine ambao huwa wanafanya sherehea kubwa kiongozi huyo huwa anaitumia siku hiyo kwa kupumzika huku akipokea ujumbe mbalimbali wa kumtakia kila la kheri.

Alisema kuwa kama jana kiongozi huyo alipokea salamu mbalimbali kutoka kwa viongozi wan je na miongoni mwa waliompigia simu ni Rais wa  Belarusi,  Alexander Lukashenko, Rais wa Azerbaijani,  Ilham Aliyev  na wa  Armenia, Armen Sarkissian.

Alisema kwamba pia Waziri Mkuu,  Dmitry Medvedev  alimpigia simu Rais  Putin  akimtakia afya njema na mafanikio makubwa kwa kazi anayoifanya kwa ajili ya maslahi ya wananchi wan chi hii.

Mwaka jana Rais  Putin aliitumia siku hiyo akiwa nje ya mji huu ambapo aliamua kukutana na maofisa wa  Baraza la Usalama mkutano ambao ulifanyika mjini  Sochi.

Mwaka  2016, pia Rais Putin aliitumia siku kama hiyo bila kufanya shughuli yoyote ikiwa ni baada ya mwaka mmoja kwenda kushuhudia mechi ya mpira wa magongo na huku mwaka 2014 akiisherehekea akiwa ziarani nchini Siberian.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles