VATICAN CITY,Vatican
KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amesema kwamba ukimya juu ya unyanyasaji wa kijinsia hauwezi kuvumiliwa na ndio maana ameagiza uchunguzi ufanyike juu ya aliyekuwa Askofu Mkuu wa Jimbo la Washington, Theodore McCarrick, ambaye alijiuzulu mwezi Julai mwaka huu.
Kauli hiyo ya Papa ni tamko rasmi la Vatican ambalo limetangaza kwamba Kanisa lilipaswa kukabiliana na tatizo kubwa la unyanyasaji kijinsia ndani na nje ya chombo hicho cha imani.
Taarifa hiyo ya Vatican iliyotolewa juzi ilieleza kwamba Papa Francis anafahamu na kusononeshwa na uchafu huo na shutuma zinavyosababisha aibu kwa watumishi wa kanisa hilo.
“Vikwazo vyote na mizizi yake haviwezi tena kuvumiliwa na Kanisa lilikuwa na wajibu kuzuia uhalifu huo usiojitokeza katika siku zijazo kwa watu wasiokuwa na hatia zaidi na walioathirika zaidi katika jamii,”ilieleza taarifa ya kiongozi huyo.
Taarifa hiyo pia imesisitiza kwamba pia Papa Francis katika barua ya ujumbe ambao aliutuma Agosti kwa wakatoliki wote alieleza kwamba njia pekee ambayo tunapaswa kuitumia kukomesha uovu huu  huu ambao umesitisha maisha ya wengi sana ni kutambua kuwa sisi sote ni watoto wa Mungu.
“Uelewa huu ukiwa sehemu ya watu na historia iliyoshirikishwa itatusaidia kutambua dhambi na makosa yetu ya zamani kwa uwazi wa uhalifu ambao unaweza kutuwezesha kusavishika upya ndani ya nafsi zetu,” alieleza taarifa hiyo.