23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

IMANI ZA USHIRIKINA ZAKIMBIZA WALIMU

 

 

Na ANNA RUHASHA

SHULE ya Msingi Bongonya wilayani Sengerema   inakabiliwa na upungufu wa walimu  baada  ya  baadhi yao   kuihama shule   kwa madai ya  kukithiri  ushirikina.

Kwa mujibu wa walimu hao, hali hiyo  imekuwa ikichangia wanafunzi kuanguka ovyo pamoja na kuwapo fisi wengi.

Hayo yalielezwa   wakati wa  ziara ya Mbunge wa   Sengerema, William Ngeleja   kukagua shughuli za maendeleo  akiwa na Kaimu  Ofisa Elimu Msingi  wa Wilaya hiyo, Theobadia Katama.

Ilielezwa kuwa   shule hiyo hivi sasa  ina    walimu   saba   wakiume  na   upungufu wa walimu 10.

Katama alisema   kilichosababisha  shule hiyo kukosa walimu ni pamoja na waliokuwapo  kuomba  uhamisho  wa lazima  kutokana na mazingira    shuleni hapo ya   kuanguka  wanafunzi na kuzingirwa na fisi  katika maeneo  wanayofanyia kazi.

‘‘Ndugu wananchi  hapa  shuleni tulikuwa na walimu wengi lakini waliomba uhamisho baada  kuhofia usalama wa  maisha yao.

“Hao walimu walikuwa  wanasema wasipohamishwa  wanaacha kazi… haka  kamchezo kaishe vinginevyo hatutapata walimu wa kutosha hapa, ’’ alisema Katama.

Kaimu  Mwalimu Mkuu wa shule  hiyo, Elias George,  alisema  shule   ina   wanafunzi 800  na       walimu wamekuwa na mzigo mkubwa wa kukabiliana na vipindi.

Alisema  kila mwalimu  ana zaidi ya vipindi 30   hivyo akaiomba  a serikali kutatua changamoto hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya wazazi,  Stansilaus  Costantine  alisema  matukio ya kuanguka  yamekuwa yakiwakuta wanafunzi na siyo walimu.

Alisema   walimu walitumia  kigezo hicho labda kwa kuona shule haina miundombinu rafiki kwao.

Mbunge wa   Sengerema,william Ngereja,  akizungumza  na wananchi wa kijiji hicho   alisema tatizo hilo litatatuliwa kwa  dua na sala  za mashekh na mapadri kukemea mapepo hayo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles