25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

10 wanusurika kifo, mmoja hajulikani alipo boti ikizama Tanga

Oscar Assenga, Tanga

Watu 10 wamenusufika kifo huku mmoja akiwa hajulikani alipo baada ya boti waliyopanda kuzama kwenye Bahari ya Hindi Jijini Tanga, walipokuwa wakienda kuangalia visiwa vilivyopo baharini humo.

Akizungumza leo na Mtanzania Digital leo Jumatatu Agosti 12,  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema limetokea jana ambao walikuwa  watu hao walikuwa wamepanda boti waliyokodi kutoka eneo la Yatch Club.

“Baada ya watu hao kupanda boti hiyo, ambao walikuwa wakienda kutembelea visiwa mbalimbali vilivyopo kwenye bahari hiyo na ndipo upepo mkali uliwazuia kwenda mbele na walipotaka kugeuza kurudi walipotoka ndipo ilipopinduka na kuwamwaga.

“Kwenye boti hiyo kulikuwa na watu 11 ambapo 10 kati yao waliokolewa kutokana na kuvaa maboya wakati wakiwa baharini na mwingine mmoja ambaye inadaiwa hakuwa nayo hadi sasa hajulikani alipo,” amesema.

Aidha, Kamanda Bukombe ametoa wito kwa wananchi wanaotumia bahari kusafiria kuchukua tahadhari wanapokuwa baharini kwa kuhakikisha wanavaa maboya ya kujiokolea ili wakati yanapotokea majanga kama hayo waweze kuona namna ya kujiokoa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles