27.9 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Sheikh Dodoma ataka asilaumiwe mtu ajali Morogoro

Ramadhan Hassan, Dodoma

Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Mustapha Rajabu amewaomba Watanzania kuwaombea waliofariki na majeruhi wa ajali ya moto ilivyotokea mkoani Morogoro juzi Jumamosi Agosti 10.

Aidha, amesema hakuna wa kulaumiwa kutokana na tukio hilo ambapo watu zaidi ya 65 na walifariki dunia.

Akizungumza leo Jumatatu Agosti 12, katika Ibada ya Iddi El Hajj iliyofanyika katika Msikiti wa Gaddaf Jijini hapa, Sheikh Rajabu amesema hakuna wa kumlaumu katika ajali hiyo kwani kila mmoja Mwenyezi Mungu amempanguia namna ambavyo atafariki.

“Kutokana na ile ajali nani wa kulaumiwa, hakuna wa kulaumiwa, hatupaswi kulalamika, Mwenyezi Mungu amepanga kila mmoja atakufa kwa namna ambayo atakuwa amepanga yeye.

“Kuna wengine watakufa kwa upanga,kuna wengine watakufa majini na kwenye ajali kwa hiyo hakuna wa kulaumiwa katika hili,” amesema.

Aidha aliipongeza Serikali kwa kuwasaidia majeruhi wa ajali hiyo pamoja na kuwahifadhi wale ambao wamefariki.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles