25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, May 2, 2024

Contact us: [email protected]

Wanariadha wanawake kuchuana mashindano ya ‘Ladies First’

Na Winfrida Mtoi, Mtanzania Digital

Wanariadha  wanawake kutoka mikoa 31 ya Tanzania Bara na Zanzibar, wanatarajiwa kuchuana  katika mashindano ya riadha ya tamasha  la ‘Ladies First’ kuanzia  Novemba 24 hadi 26, 2023, jijini Dar es Salaam. 

Tamasha hilo ambalo muasisi wake ni mwanariadha mkongwe, Juma Ikangaa, linafanyika kwa msimu wa tano sasa, likidhaminiwa na Shirikala Maendeleo la Kimataifa la Japani (JICA) na kuratibiwa na Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

Mwakilishi Mkuu wa JICA Tanzania, Ara Hitoshi (katika), akizungumza na waandishi wa habari leo Novemba 22,2023, Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa(BMT), Neema Msitha(kulia) na Muasisi wa Ladies First, Juma Ikangaa(kushoto).

Akizungumza na waandishi wa habari leo Novemba 22, 2023, Dar es Salaam wakati wa kutangaza mashindano hayo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa(BMT), Neema Msitha amesema mgeni rasmi siku ya ufunguzi atakuwa  Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Damas Ndumbaro.

Amesema ufunguzi rasmi utafanyika Novemba 25, pia kutakuwa na wageni mbalimbali walioshirikiana nao kuandaa tamasha hilo, akiwemo balozi wa Japani na viongozi wa juu wa JICA ambao ni wadhamini wakuu wa mashindano hayo.

Katibu huyo amesema pamoja na mashindano ya riadha, watafanya mafunzo na semina  za ujasiriamali na uongozi kwa wanamichezo wote watakaoshiriki tamasha hilo.

“Tunafahamu wachezaji wanacheza lakini inafika kipindi wanastaafu, tumeona tuwape elimu hii ya ujasiliamali  ili kuweza kujiokoa kimaisha  hata baada ya kumaliza shughuli za michezo,”amesema.

Naye  Mwakilishi Mkuu wa JICA Tanzania, Ara Hitoshi, amesema mashindano ya ‘Ladies First ni muendelezo wa  kutengeneza usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake kupitia michezo.

Amesema anaamini michuano hiyo itatoa fursa kwa wanawake kufikia  malengo ya usawa kwenye michezo na kuonyesha kile walichofanyia mazoezi kwa muda mrefu.

“Kupitia mashindano haya, Watanzania hasa wanawake na wasichana watapata msukumo wa kimichezo na  wataongeza uelewa  wao kuhusu umuhimu wa usawa wa kijinsia na uwezeshaji,” amesema Hitoshi.

Kwa upande wake mwakilishi wa Shirikisho la Riadha nchini(RT), Michael Washa, ametaja michezo itakayokuwepo siku hiyo kuwa  ni kurusha mkuki, kupokezana vijiti na mbio za kuanzia mita 100, 200, 400,800, 1500, 5000 na 10,000.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles