25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Snura: Natarajia kutoa filamu mwakani

Snura Mushi
Snura Mushi

NA FESTO POLEA,

MSANII Snura Mushi ‘Snura Majanga’, aliyewahi kuwika na nyimbo mbalimbali, ameibuka na kudai kwamba ana mpango wa kutoa filamu moja mwakani.

Snura alisema baada ya kuingia katika muziki amekuwa na shoo nyingi kiasi kwamba hukosa muda wa kuigiza, licha ya mashabiki wake kumtaka afanye hivyo hata kwa mara moja.

“Mashabiki wangu wamekuwa wakinitaka angalau nicheze hata filamu nmoja, lakini shoo za muziki zimekuwa nyingi nakosa muda wa kuigiza, lakini nitapanga mwakani nitoe filamu moja kwa ajili ya mashabiki wangu huku nikiendelea na muziki,’’ alisema Snura, ambaye amekuwa akiingiza fedha nyingi kupitia shoo zake za mara kwa mara mikoa mbalimbali.

Snura ameigiza filamu mbalimbali na mwanzo wa safari yake ya sanaa aliwahi kuwa kundi moja na marehemu Sharo Milionea na Kitale.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles